4/04/2018

Swahili Christian Movie "Maskani Yangu Yako Wapi" | Mungu ni Kimbilio la Nafsi Yangu

Swahili Christian Movie“Maskani Yangu Yako Wapi”| Mungu ni Kimbilio la Nafsi Yangu


Wazazi wa Wenya walitengana alipokuwa na umri wa miaka miwili, na baada ya hapo aliishi na baba yake na mama wa kambo. Mamake wa kambo hakuweza kumvumilia na daima alikuwa akibishana na baba yake. Alikuwa na chaguo dogo — alilazimika kumpeleka Wenya nyumbani kwa mama yake, lakini mama yake alilenga kikamilifu kuendesha biashara yake na hakuwa na muda wa kumtunza Wenya, hivyo mara nyingi alipelekwa nyumbani kwa jamaa na marafiki zake kupata ulezi.

4/03/2018

Kuendeleza Ubora wa Tabia ni Kwa Ajili ya Kupokea Wokovu wa Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu

Kuendeleza Ubora wa Tabia ni Kwa Ajili ya Kupokea Wokovu wa Mungu

Kuendeleza ubora wa tabia ya watu kunahitaji kwamba muendeleze uwezo wenu wa kupokea. Hitaji la msingi kabisa kwenu ni kwamba myapokee waziwazi maneno yanayonenwa kwenu. Je, siyo imani iliyovurugika ikiwa unanifuata bila kufahamu kile Ninachosema? Ubora wenu wa tabia ni duni sana. Ni kwa sababu hammiliki uwezo wa kupokea kwamba hamna ufahamu hata mdogo wa kile kinachosemwa. Kwa hivyo, ni vigumu sana kutimiza matokeo yanayotamanika. 

4/02/2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Tafuteni Maana ya Maisha - "Kwa Ajili ya Nani Mtu Aishi" (Video Rasmi ya Muziki)

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Tafuteni Maana ya Maisha - "Kwa Ajili ya Nani Mtu Aishi" (Video Rasmi ya Muziki)


Kwa Ajili ya Nani Mtu Aishi
Haikuwa wazi ni kwa ajili ya nani mtu anapaswa kuishi. Sasa nina jibu kwa hilo. Nilikuwa naishi tu kwa ajili yangu mwenyewe, kutafuta hadhi tu na umaarufu. Maombi kwa Mungu yaliyojaa maneno mema, lakini nikishikilia njia zangu mwenyewe katika maisha halisi. Imani juu ya msingi wa kesho na majaliwa, sina ukweli au uhalisi. Mila na sheria, zikifungia imani yangu; sikubaki na kitu ila utupu. Kushindwa kuishi kama binadamu, sistahili upendo wa Mungu kwa ajili yangu.

4/01/2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (10)

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (10)

Kwa wanadamu kuendelea mbele kiasi hiki ni hali isiyo na kigezo. Kazi ya Mungu na kuingia kwa mwanadamu vinaendelea bega kwa bega, na hivyo kazi ya Mungu, pia, ni tukio kubwa lisilo na kifani. 

3/31/2018

Kulipa Gharama ili Kupata Ukweli ni Muhimu Sana

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Kulipa Gharama ili Kupata Ukweli ni Muhimu Sana


Mwenyezi Mungu alisema, Sio rahisi kwa vijana kuendeleza kazi; wengi wao hawadumishi mwendo. Ni lazima moyo wako uwe mtulivu, lazima uweze kudumisha mwendo na uwe tayari kutumia muda kwake. Wengine hujiburudisha au kuwachezea wengine, lakini wewe unasema, "Siwezi, sina wakati.

3/30/2018

Namna Petro Alivyopata Kumjua Yesu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Namna Petro Alivyopata Kumjua Yesu


Katika kipindi kile ambacho Petro alikuwa na Yesu, aliona sifa nyingi za kupendeza ndani ya Yesu, hali nyingi zenye za kustahili kuigwa, na nyingi ambazo zilimkimu. Ingawa Petro aliona nafsi ya Mungu ndani ya Yesu katika njia nyingi, na kuona sifa nyingi za kupendeza, mara ya kwanza hakumjua Yesu. Petro alianza kumfuata Yesu alipokuwa na umri wa miaka 20, na akaendelea kufanya hivyo kwa miaka sita. 

3/29/2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Ufafanuzi wa Tamko la Sita

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Ufafanuzi wa Tamko la Sita

Binadamu wanapigwa bumbuazi kwa sababu ya matamshi ya Mungu wanapotambua kwamba Mungu amefanya kitendo kikubwa katika ulimwengu wa kiroho, kitu ambacho mwanadamu hawezi na ambacho Mungu Mwenyewe pekee ndiye Anaweza kufanikisha. Kwa sababu hii, Mungu mara tena anawasilisha maneno ya huruma kwa wanadamu. Mioyo ya watu inapojaa ukinzani, ikishangaa: “Mungu ni Mungu asiye na huruma au upendo, lakini badala yake Mungu aliyejitolea kuwaangusha binadamu; kwa hiyo mbona Atuonyeshe huruma? Yawezekana kwamba Mungu kwa mara nyingine amehamia kwa utaratibu?” wakati ambapo fikira hii, wazo hili huumbika ndani ya akili zao, wao hung’ang’ana kulishinda kwa nguvu zao zote.