Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Vitabu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Vitabu. Onyesha machapisho yote

9/28/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 111


Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 111


Mataifa yote yatabarikiwa kwa sababu Yako; watu wote watanikaribisha kwa shangwe na kunisifu kwa sababu Yako. Ufalme Wangu utafanikiwa na kukua, na utabaki milele. Hakuna mtu ataruhusiwa kuukanyaga na hakuna kitu kitaruhusiwa kuwepo ambacho hakikubaliani na Mimi, kwa sababu Mimi ni Mungu mwenye uadhama na asiyekosewa Mwenyewe. Sikubali mtu yeyote anihukumu na Sikubali mtu yeyote kutolingana na Mimi. Hili linatosha kuonyesha tabia Yangu na uadhama Wangu.

9/25/2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 110

Sauti ya Mungu | Sura ya 110


Kila kitu kitakapofichuliwa utakuwa wakati ambapo Nitapumzika, na hata zaidi, utakuwa wakati ambapo kila kitu kitakuwa sawa. Mimi hufanya kazi Yangu binafsi; Mimi hupanga kila kitu na kusafidi kila kitu Mwenyewe. Nitakapotoka Sayuni na Nitakaporejea, wazaliwa Wangu wa kwanza watakapokuwa wamekamilishwa na Mimi, Nitakuwa Nimemaliza kazi Yangu kubwa. Katika mawazo ya watu kitu ambacho kinafanywa ni sharti kiweze kuonekana na kuguswa, lakini jinsi Ninavyoona, kila kitu ni kikamilifu wakati ambapo Ninafanya mpango Wangu.

9/22/2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 109


Maneno ya Mungu | Sura ya 109


Ninatoa matamko kila siku, kuzungumza kila siku, na kufichua ishara Zangu kuu na shani kila siku. Haya yote ni kazi ya Roho Wangu. Machoni pa watu Mimi ni mwanadamu tu, lakini hasa ni katika mwanadamu huyu ndipo Ninafichua vyote Vyangu na nguvu Yangu kuu.

Kwa kuwa watu humpuuza mwanadamu Niliye na huyapuuza matendo Yangu, wanafikiri kuwa hivi ni vitu ambavyo hufanywa na wanadamu. Lakini mbona hufikiri: Je, watu wanaweza kutimiza yale Ninayoyatenda? 

9/19/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 108


Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 108


Ndani Yangu, wote wanaweza kupata raha na wote wanaweza kuwa huru. Wale walio nje Yangu hawawezi kupata uhuru na furaha kwa sababu Roho Wangu hayuko pamoja na watu hawa. Watu hawa wanaitwa wafu wasio na roho. Nami Nawaita wale walio ndani Yangu watu walio hai wenye roho. Wao ni Wangu, na watarudi kwenye kiti Changu cha enzi. Wale ambao hutoa huduma na wale ambao ni wa ibilisi ni wafu wasio na roho, nao wanapaswa kuangamizwa hadi wawe katika hali ya kutokuwepo.

9/10/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 107

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 107


Wakati maneno Yangu ni makali kwa kiwango fulani, watu wengi huondoka kwa sababu ya maneno Yangu. Ni wakati huu hasa ambapo wazaliwa Wangu wa kwanza wanafichuliwa. Nimesema kuwa Sitafanya lolote, lakini Nitatumia tu maneno Yangu kutimiza mambo yote. Ninatumia maneno Yangu kuwaangamiza wote ambao Ninawachukia, na pia Ninatumia maneno Yangu kuwakamilisha wazaliwa Wangu wa kwanza. (Maneno Yangu yatakaponenwa, ngurumo saba zitatoa sauti, na wakati huo wazaliwa Wangu wa kwanza pamoja na Mimi tutabadili sura na kuingia katika ulimwengu wa kiroho.) Niliposema Roho Wangu hufanya kazi binafsi, Nilichomaanisha ni kuwa maneno Yangu hutimiza yote, na kupitia kwa hili mtu anaweza kuona kwamba Mimi ni mwenyezi.

9/07/2019

Matamshi ya Kristo | Sura ya 106

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Kristo | Sura ya 106


Wale wasioyajua maneno Yangu, wale wasioujua ubinadamu Wangu wa kawaida, na wale wanaokataa uungu Wangu wote wataangamizwa hadi wasikuwepo. Hakuna atakayeachiliwa kutokana na hili, na wote lazima wapitie hili kwa sababu ni amri Yangu ya utawala, na ndicho kifungu kikali zaidi cha amri Yangu. Wale wasioyajua maneno Yangu ni wale ambao wamesikiliza yale ambayo Nimesema wazi, ilhali bado hawayajui, kwa maneno mengine wale ambao hawaelewi masuala ya kiroho (kwa kuwa Sijaumba sehemu hii ya mwili kwa ajili ya wanadamu, Sihitaji mengi kutoka kwao; Nahitaji tu kwamba wasikilize maneno Yangu na kisha wayaweke katika matendo).

9/04/2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 105

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu


Maneno ya Mungu | Sura ya 105

Kwa sababu ya kanuni za maneno Yangu, kwa sababu ya utaratibu wa kazi Yangu, watu hunikana; hili ndilo kusudi Langu la kuzungumza kwa muda mrefu (imezungumzwa kuhusu wazao wote wa joka kubwa jekundu). Ni njia ya hekima ya kazi Yangu; ni hukumu Yangu ya joka kubwa jekundu; huu ni mkakati Wangu, hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuuelewa kikamilifu. Katika kila kipindi muhimu, yaani, katika kila awamu ya mpito ya mpango Wangu wa usimamizi, baadhi ya watu lazima waondolewe; wanaondolewa kulingana na utaratibu wa kazi Yangu.

9/01/2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 104

Sauti ya Mungu | Sura ya 104

Watu, matukio na vitu vyote nje Yangu vitakufa na kuwakatika hali ya kutokuwepo, ilhali watu, matukio na vitu vyote vilivyo ndani Yangu vitapata kila kitu kutoka Kwangu na kuingia katika utukufu pamoja na Mimi, kuingia katika Mlima Wangu Sayuni, makazi Yangu, na kuishi pamoja kwa amani nami milele. Niliumba vitu vyote mwanzoni na Nitamaliza kazi Yangu mwishowe, na pia Nitatawala milele kama Mfalme.

8/29/2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 103

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Maneno ya Mungu | Sura ya 103

Sauti ya mngurumo inatoka, ikiutetemesha ulimwengu mzima, ikiwahanikiza watu, na kuwafanya wachelewe kukwepa, na wengine wanauawa, baadhi wanaangamizwa, na wengine wanahukumiwa. Kweli ni kioja ambacho hakuna yeyote amewahi kukiona awali. Sikiliza kwa makini, milio ya radi inafuatana na sauti za kuomboleza, na sauti hii inatoka kuzimu, sauti hii inatoka jahanamu. Ni sauti yenye uchungu ya wale wana wa uasi ambao wamehukumiwa nami. Wale wasiosikiza kile Ninachosema na hawatendi maneno Yangu wanahukumiwa vikali na kupokea laana ya ghadhabu Yangu.

8/20/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 102

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 102

Nimeongea hadi kwa kiwango fulani na kufanya kazi hadi kwa kiwango fulani; ninyi nyote mnapaswa kuelewa mapenzi Yangu na kwa viwango tofauti muweze kuzingatia mzigo Wangu. Sasa ndicho kipindi muhimu kutoka katika mwili kuingia katika dunia ya roho, na ninyi ndio watangulizi kwa kutagaa enzi, wanadamu wa ulimwengu wanaovuka miisho ya ulimwengu. Ninyi ni wapendwa Wangu zaidi; ninyi ndio Ninaowapenda. Inaweza kusemwa kwamba Sina wapendwa wengine ila ninyi, kwa sababu jitihada Yangu yote ya bidii imekuwa kwa ajili yenu—inaweza kuwa kwamba hamjui hilo?

8/17/2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 101

Mwenyezi Mungu,Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki

Sauti ya Mungu | Sura ya 101

Sitakuwa mwenye huruma kwa yeyote anayeingilia usimamizi Wangu ama anayejaribu kuiharibu mipango Yangu. Kila mtu anapaswa kuelewa kile Ninachomaanisha kutoka kwa maneno Ninayosema na lazima aelewe vizuri kile Ninachozungumzia. Kwa kuzingatia hali iliyopo, kila mtu anapaswa kujichunguza: Ni wajibu gani unaotekeleza? Unaishi kwa ajili Yangu, au unamtumikia Shetani? Je, kila moja ya matendo yako hutoka Kwangu, au hutoka kwa Shetani? 

8/14/2019

Matamshi ya Kristo | Sura ya 100

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Kristo | Sura ya 100

Ninawachukia wale wote ambao hawajajaaliwa na kuchaguliwa na Mimi. Kwa hiyo ni lazima Niwafukuze watu hawa kutoka katika nyumba Yangu mmoja baada ya mwingine, hivyo hekalu Langu litakuwa takatifu na bila doa, nyumba Yangu itakuwa mpya daima na haitakuwa nzee kamwe, jina Langu takatifu litaenezwa milele na watu Wangu watakatifu watakuwa wapendwa Wangu. Aina hii ya mandhari, aina hii ya nyumba, aina hii ya ufalme ni lengo Langu, makao Yangu nayo ni msingi wa uumbaji Wangu wa vitu vyote. 

8/11/2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 99

Maneno ya Mungu | Sura ya 99

Kwa sababu mwendo wa kazi Yangu unaongeza kasi, hakuna anayeweza kuenda mwendo sawa na nyayo Zangu, na hakuna anayeweza kupenya akili Yangu, lakini hii ndiyo njia tu ambayo lazima isafiriwe. Hii ni “wafu” yaani wakati Ninapoongea kuhusu kufufuliwa kutoka kwa wafu (inarejelea kukosa uwezo wa kufahamu mapenzi Yangu, kukosa uwezo wa kuelewa kile Ninachomaanisha kutoka kwa maneno Yangu. Haya ni maelezo mengine ya “wafu”, na hayamaanishi kutelekezwa na Roho Wangu).

8/08/2019

Kumwamini Mungu Kunapaswa Kulenge Uhalisi, Si Kaida za Kidini

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Kumwamini Mungu Kunapaswa Kulenge Uhalisi, Si Kaida za Kidini

Je, ni desturi ngapi za kidini unazozizingatia? Ni mara ngapi umeasi dhidi ya neno la Mungu na kwenda kwa njia yako? Ni mara ngapi umetia katika vitendo neno la Mungu kwa sababu kwa kweli unajali mizigo Aliyobeba na unatafuta kutimiza mapenzi Yake? Lielewe neno la Mungu na uliweke katika vitendo. Kuwa mwenye maadili katika vitendo na matendo yako; huku si kutii sheria au kufanya hivyo shingo upande kwa ajili ya kujionyesha.

7/30/2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 98

Maneno ya Mungu | Sura ya 98

Mambo yote yatakuja juu ya kila mmoja wenu, na yatawawezesha kujua zaidi juu Yangu na kuwa na uhakika zaidi juu Yangu. Yatawawezesha kunijua, Mungu mmoja Mwenyewe, kunijua Mimi Mwenye uweza, kunijua Mimi Mungu Mwenyewe mwenye mwili. Baadaye, Nitatoka katika mwili, Nirudi Sayuni, Nirudi katika nchi nzuri ya Kanaani, ambayo ni makazi Yangu, ndiyo hatima Yangu, na ndio msingi ambao niliumba vitu vyote.

7/27/2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 97

Umeme wa Mashariki,Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu

Sauti ya Mungu | Sura ya 97
Nitafanya kila mtu aone matendo Yangu ya ajabu na kusikia maneno Yangu ya hekima. Ni lazima iwe kila mtu na ni lazima iwe juu ya kila suala. Hii ni amri Yangu ya utawala na ni ghadhabu Yangu. Nitahusisha kila mtu na kila jambo ili watu wote kutoka mwisho mmoja wa ulimwengu hadi mwingine wataona kwa macho yao wenyewe, la sivyo Sitaacha kamwe. Ghadhabu Yangu imemwagwa kikamilifu na hakuna hata chembe imezuiwa. Inaelekezwa kwa kila mtu mmoja ambaye anakubali jina hili (hivi karibuni itageuzwa juu ya mataifa yote ya dunia).

7/24/2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 96

Maneno ya Mungu | Sura ya 96

Nitamwadibu kila mtu aliyezaliwa kutoka Kwangu ambaye bado hanijui ili kuonyesha ghadhabu Yangu yote, kuonyesha nguvu Zangu kuu, na kuonyesha hekima Yangu kamili. Ndani Yangu kila kitu ni chenye haki na bila shaka hakuna udhalimu, hakuna udanganyifu, na hakuna upotovu; yeyote ambaye ni mpotovu na mdanganyifu lazima awe ni mwana wa jahanamu—lazima amezaliwa huko kuzimu. 

7/21/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 95

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 95
Watu hufikiri kila kitu kuwa rahisi sana, wakati kwa kweli hali siyo hivyo. Ndani ya kila kitu kuna siri zilizofichwa, na vile vile hekima Yangu na mipango Yangu. Hakuna utondoti usioangaliwa, na yote yanapangwa na Mimi Mwenyewe. Hukumu ya siku kuu inawafikia wale wote wasionipenda kwa kweli (kumbuka, hukumu ya siku kuu inalenga kila mtu anayepokea jina hili) na kuwasababisha kulia na kusaga meno.

7/16/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 94

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 94

Narudi Sayuni pamoja na wazaliwa Wangu wa kwanza—kweli mnaelewa maana ya kweli ya maneno haya? Nimewakumbusha tena na tena kwamba Mimi nataka mkue haraka ili mtawale na Mimi. Je, mnakumbuka? Vitu hivi vyote vinahusiana moja kwa moja na kupata mwili Kwangu. Kutoka Sayuni Nilikuja duniani katika nyama ili Nipate kupitia nyama kundi la watu ambao ni wa akili moja na Mimi, na kisha turudi Sayuni.

7/13/2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 93

Sauti ya Mungu | Sura ya 93

Ukweli unatimizwa mbele ya macho ya mtu na mambo yote yametimizwa. Kazi Yangu inapata hatua, ikipanda juu kama roketi iliyofyatuliwa, ambayo hakuna mtu aliwahi kutarajia. Ni baada ya vitu kufanyika ndipo mtaelewa maana ya kweli ya maneno Yangu. Watoto wa joka kubwa jekundu si wa pekee na lazima wafanywe kushuhudia matendo Yangu ya ajabu kwa macho yao wenyewe. Usidhani kwamba Sitakutelekeza, sasa kwa kuwa una uhakika kunihusu baada ya kuona matendo Yangu—si rahisi hivyo!