3/08/2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VIII Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (II)” Sehemu ya Pili



Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VIII Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (II)” Sehemu ya Pili


Mwenyezi Mungu anasema, “Tofauti kubwa kabisa kati ya Mungu na wanadamu ni kwamba Mungu hutawala vitu vyote na hupeana vitu vyote. Mungu ni chanzo cha vitu vyote, na wanadamu hufurahia vitu vyote wakati Mungu anawapa. Hiyo ni kusema, mwanadamu hufurahia vitu vyote anapokubali maisha ambayo Mungu anatoa kwa vitu vyote. Wanadamu hufurahia matokeo ya uumbaji wa Mungu wa vitu vyote, ilhali Mungu ni Bwana.

3/06/2019

“Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VIII Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote II” Sehemu ya Kwanza


Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VIII Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote II” Sehemu ya Kwanza


Mwenyezi Mungu anasema, “Mungu aliumba vitu vyote na akatumia mbinu Zake kutunga sheria za ukuaji wa vitu vyote, na vilevile njia na mpangilio wa ukuaji wa vitu hivyo, na pia alitunga njia za kuwepo kwa vitu vyote duniani, ili viweze kuishi kwa kuendelea na kutegemeana. Kwa mbinu na sheria hizi, vitu vyote vinaweza kuwepo na kukua katika nchi hii kwa ufanisi na kwa amani. Ni kwa kuwa tu na mazingira kama haya ndipo wanadamu wanaweza kuwa na makao na mazingira ya kuishi yaliyo thabiti, na chini ya uongozi wa Mungu, waendelee kukua na kusonga mbele, kukua na kusonga mbele.”

kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Yaliyopendekezwa: Kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu

3/04/2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Kazi ya Kueneza Injili Ni Kazi ya Kuokoa Binadamu Pia”


Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Kazi ya Kueneza Injili Ni Kazi ya Kuokoa Binadamu Pia”


Mwenyezi Mungu anasema, “Ili kwamba katika enzi hii ya mwisho jina Langu litatukuzwa miongoni mwa Mataifa, kwamba matendo Yangu yataonekana na mataifa mengine na wataniita Mwenyezi kwa sababu ya matendo Yangu, na kwamba maneno Yangu yatatimika karibuni. Nitawafanya watu wote wajue kwamba Mimi siye tu Mungu wa Waisraeli, lakini Mimi ni Mungu wa Mataifa yote, hata mataifa yale Niliyoyalaani.

3/03/2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Unapaswa Kutayarisha Matendo Mema ya Kutosha kwa ajili ya Hatima Yako”


Maneno ya Roho Mtakatifu | “Unapaswa Kutayarisha Matendo Mema ya Kutosha kwa ajili ya Hatima Yako”


Mwenyezi Mungu anasema, “Huruma Zangu zinaonyeshwa kwa wale wanaonipenda Mimi na kujinyima wenyewe. Na adhabu inayoletwa kwa waovu ni thibitisho hasa la tabia Yangu ya haki na, zaidi sana, ushuhuda wa hasira Yangu. Msiba utakapokuja, njaa na baa litawakumba wale wote wanaopinga Mimi na watalia kwa uchungu. Wale wote ambao wametenda aina zote za uovu, lakini ambao wamenifuata kwa miaka mingi, hawataepuka shtaka rasmi lililoandikwa; wao pia, wakijipata katika maafa, ambayo yameonekana kwa nadra katika enzi zote, wataishi katika hali ya kila siku ya taharuki na woga.

3/01/2019

Wimbo wa Kusifu na Kuabudu 2019 | “Watu wa Mungu wa Mataifa Yote Huonyesha Hisia Zao Kama Mtu Mmoja”


Wimbo wa Kusifu na Kuabudu 2019 | “Watu wa Mungu wa Mataifa Yote Huonyesha Hisia Zao Kama Mtu Mmoja”


Uangalie ufalme wa Mungu, ambako Mungu anatawala juu ya yote.
Kutoka wakati uumbaji ulipoanza mpaka siku ya sasa,
wana wa Mungu waliongozwa wakipitia taabu.
Katika milima na mabonde walienda. Lakini sasa katika nuru Yake wanakaa. 
  Nani asiyelia juu ya udhalimu wa jana?
Ni nani asiyelia machozi kwa ajili ya maisha magumu leo?
Ni nani asiyechukua nafasi hii kutoa mioyo yao kwa Mungu?
Nani hataki kutoa sauti kwa shauku na uzoefu wake?
Nani asiyelia juu ya udhalimu wa jana?
Ni nani asiyelia machozi kwa ajili ya maisha magumu leo?
Ni nani asiyechukua nafasi hii kutoa mioyo yao kwa Mungu?
Nani hataki kutoa sauti kwa shauku na uzoefu wake?

2/28/2019

Neno la Mungu | Sura ya 27

Mungu mmoja wa kweli anayetawala vitu vyote katika ulimwengu—Kristo mwenyezi! Huu ndio ushuhuda wa Roho Mtakatifu, ni ushahidi dhahiri! Roho Mtakatifu anafanya kazi kuwa na ushuhuda kila mahali, ili kusiwe na mtu yeyote mwenye shaka yoyote. Mfalme wa ushindi, Mwenyezi Mungu! Yeye ameushinda ulimwengu, Ameishinda dhambi na kufanikisha ukombozi! Anatuokoa, kundi hili la watu ambao wamepotoshwa na Shetani, na Anatukamilisha kutekeleza mapenzi Yake. Anatawala dunia nzima, Anaichukua tena na kumfukuza Shetani hadi ndani ya shimo lisilo na mwisho. Anauhukumu ulimwengu, na hakuna mtu anayeweza kukwepa kutoka mikononi Mwake. Anatawala kama Mfalme.

Neno la Mungu | Sura ya 26

Wanangu, yatilieni maanani maneno Yangu, sikiliza kwa utulivu sauti Yangu na Nitafichua kwako. Uwe na utulivu ndani yangu, kwa maana Mimi ni Mungu wako, Mkombozi wenu wa pekee. Mnatakiwa kutuliza mioyo yenu nyakati zote, mkae ndani yangu; Mimi ni mwamba wako, msaidizi wenu. Msiwe na nia nyingine, lakini mnitegemee kwa mioyo yenu yote na Mimi nitaonekana kwenu kwa hakika—Mimi ni Mungu wenu! Ah, wale wenye mashaka! Hakika hawawezi kusimama imara na hawatapata chochote. Lazima mjue sasa ni wakati gani, ni wakati muhimu kiasi gani.