Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Utangulizi. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Utangulizi. Onyesha machapisho yote

12/14/2018

Matamshi na Ushuhuda wa Kristo Mwanzoni|Utangulizi

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki


Matamshi na Ushuhuda wa Kristo Mwanzoni|Utangulizi 


Mnamo Februari 11, mwaka wa 1991, Mungu alitoa tamko Lake la kwanza katika kanisa ambalo lilikuwa na athari isiyo ya kawaida kwa kila mmoja wa watu walioishi katika mkondo wa Roho Mtakatifu wakati huo. Tamko hili lilitaja yafuatayo: “Makazi ya Mungu yameonekana” na “Mkuu wa ulimwengu, Kristo wa siku za mwisho—Yeye ni Jua linalong’aa.” Kwa maneno haya ya maana sana, watu hawa wote waliletwa katika ulimwengu mpya. Wale wote waliosoma tamko hili walihisi maelezo ya kazi mpya, kazi kuu ambayo Mungu alikuwa karibu kuanzisha.