Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo manna-ya-Mwenyezi-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo manna-ya-Mwenyezi-Mungu. Onyesha machapisho yote

11/25/2017

Wale Wasiopatana Na Kristo Hakika Ni Wapinzani Wa Mungu

 Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu


Wale Wasiopatana Na Kristo Hakika Ni Wapinzani Wa Mungu



 Watu wote wana tamaa ya kuona uso wa kweli wa Yesu na kutaka kuwa pamoja Naye. Naamini kuwa hakuna mmoja wa ndugu au dada anayeweza kusema kwamba yeye hana nia ya kumwona au kuwa pamoja na Yesu. Kabla ya nyinyi kumwona Yesu, yaani, kabla ya nyinyi kumwona Mungu Aliye kwenye mwili, mtakuwa na mawazo mengi, kwa mfano, kuhusu sura ya Yesu, njia Yake ya kuzungumza, njia Yake ya maisha, na kadhalika. Hata hivyo, wakati mnamwona hasa, mawazo yenu yatabadilika haraka. Ni kwa nini? Je, mnataka kujua? Hata ingawa fikira za mwanadamu hakika haziwezi kupuuzwa, haikubaliki kamwe mwanadamu kubadilisha kiini cha Kristo.