Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo wafuasi-wa-Kristo. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo wafuasi-wa-Kristo. Onyesha machapisho yote

6/27/2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 84

Umeme wa Mashariki,Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu

Sauti ya Mungu | Sura ya 84
Kwa sababu ya ukosefu wao wa ujuzi kunihusu Mimi, mwanadamu amekatiza usimamizi Wangu na kudhoofisha mipango Yangu mara zisizo na idadi, lakini hawajawahi kuweza kuzuia hatua Zangu zinazoendelea mbele. Hii ni kwa sababu Mimi ni Mungu wa hekima. Pamoja na Mimi kuna hekima isiyo na mipaka; pamoja na Mimi kuna siri isiyo na mipaka na isiyoweza kueleweka. Mwanadamu hajawahi kuweza kuielewa na kuifahamu kabisa tangu zamani za kale hadi milele. Je, hilo haliko hivyo?