10/10/2018

Kwaheri kwa Zile Siku za Kushindana na Majaliwa

Kanisa la Mwenyezi Mungu, ushuhuda, Umeme wa Mashariki


Kwaheri kwa Zile Siku za Kushindana na Majaliwa

Yixin
Kijiji cha kishamba kilichojikokota kimaendeleo, wazazi wangu waliochoka kwa sababu ya kazi zao, maisha ya shida za kifedha … kumbukumbu hizi za huzuni zilitia alama kwa mawazo yangu machanga, zilikuwa ni hisia yangu ya kwanza ya “majaliwa.” Baada ya kuanza kwenda shule, mara ya kwanza nilipomsikia mwalimu wangu akisema kwamba “Unadhibiti majaliwa yako katika mikono yako mwenyewe,” niliweka maneno haya imara mawazoni mwangu.

10/09/2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Ubia wa Kweli

66. Ubia wa Kweli

Fang Li    Jiji la Anyang, Mkoa wa Henan
Hivi karibuni nilidhani nilikuwa nimeingia katika ubia wenye kuridhisha. Mshirika wangu na mimi tuliweza kujadili kitu chochote, wakati mwingine hata nikamwomba aonyeshe dosari zangu, na hatukupigana kamwe, hivyo nilidhani tulikuwa tumefanikisha ubia wenye kuridhisha. Lakini kama ukweli ulivyofichua, ubia wenye kuridhisha kwa kweli haukuwa kama kitu chochote nilichosadiki.

10/08/2018

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (3) - Je, Hakuna Maneno au Kazi ya Mungu Nje ya Biblia?



Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (3) - Je, Hakuna Maneno au Kazi ya Mungu Nje ya Biblia?


Utambulisho

Watu wengi katika ulimwengu wa kidini wanasadiki kwamba maneno yote ya Mungu yako ndani ya Biblia, na chochote kilicho nje ya Biblia hakina kazi Yake na maneno. Hawatafuti nje ya Biblia matamko Yake katika kurudi Kwake. Je, wataweza kukaribisha kurudi kwa Bwana kama wataendelea kushikilia wazo hili? Je, Mungu angeweza kuzuiliwa tu kwa kuongea maneno yaliyo ndani ya Biblia?

10/07/2018

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (2) - Tunawezaje Kuwa na Uhakika kuwa Bwana Yesu Tayari Amerudi?



Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (2) - Tunawezaje Kuwa na Uhakika kuwa Bwana Yesu Tayari Amerudi?


Utambulisho

Tangu makanisa yalipoanza kukumbwa na ukiwa, ndugu wengi katika Bwana wamehisi kwa uwazi ukosefu wa kazi ya Roho Mtakatifu na uwepo wa Bwana, na wote wanatamani kurudi kwa Bwana. Lakini wakati tunaposikia habari ya kwamba Bwana Yesu tayari amerudi, tunawezaje kuwa na uhakika wa hili?

Yaliyopendekezwa: Kuhusu Umeme wa Mashariki, Kujua Kanisa la Mwenyezi Mungu

10/06/2018

Mama wa "Vijijini" Akutana na Binti Mkwe wa "Mjini"

Mama wa "Vijijini" Akutana na Binti Mkwe wa "Mjini"

Liu Jie, Hunan
Maoni Tofauti, Migongano Ya Siku Zote
Mimi ni mke wa kawaida, mke mzuri na mama mwenye upendo, mimi huwatunza vizuri mume wangu na watoto wangu, mimi hufanya kazi kwa bidii na mwekevu katika kuendesha nyumba yangu, na sijawahi kamwe kutumia fedha zangu bila hadhari. Lakini kitu kisichofikirika kilinifika. Mwanangu alimuoa msichana wa kisasa ambaye kwa kweli alipenda kujifurahisha na kuvaa na kufuata mitindo ya ulimwengu. Alifuatilia na kununua chochote kilichopendwa ulimwenguni, alipoteza pesa nyingi mno, na kiasi cha pesa alichopata kila mwezi ndicho kiasi alichotumia. Kwa kuwa kulikuwa na tofauti kubwa sana katika njia zetu za kufikiria na kuishi, binti mkwe wangu na mimi daima tungegombana, tulikuwa na mabishano ya hasira, na matatizo yetu yaliendelea kuwa makali zaidi na zaidi.

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Ushuhuda, Umeme wa Mashariki

10/04/2018

Mnapaswa Kuzingatia Matendo Yenu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Mnapaswa Kuzingatia Matendo Yenu

Kulingana na vitendo na matendo katika maisha yenu, nyote mnahitaji kurasa za maneno ya kuwajaza na kuwajenga kila siku, kwani mko na upungufu mno, na ujuzi na maarifa yenu ya kupokea ni ya hali ya chini sana. Katika maisha yenu ya kila siku, mnaishi katika hali na mazingira yasiyo na ukweli ama fahamu nzuri. Hamna rasilamali ya uwepo na pia hamna msingi wa Kunijua au kujua ukweli. Imani yenu imejengwa tu juu ya ujasiri usio dhahiri au kwenye ibada za kidini na ujuzi kulingana na mafundisho ya kidini kabisa.

10/03/2018

Huku Ni Kuweka Ukweli Katika Vitendo

64. Huku Ni Kuweka Ukweli Katika Vitendo

Fan Xing    Mji wa Zhumadian, Mkoa wa Henan
Katika siku za nyuma, nilikuwa nimeunganishwa na dada mmoja kufanya kazi kwa wajibu fulani. Kwa sababu nilikuwa na majisifu na mwenye kiburi na sikutafuta ukweli, nilikuwa na mawazo kiasi ya kabla kuhusu dada huyu ambayo niliweka moyoni mwangu daima na sikuzungumza waziwazi naye. Tulipotengana, sikuwa nimeingia katika ukweli wa uhusiano wa kufanya kazi wenye kuridhisha. Baadaye, kanisa lilinipangia kufanya kazi na dada mwingine nami nikaweka azimio mbele ya Mungu: Kuanzia sasa kuendelea, sitatembea katika njia za kufeli. Nimejifunza mafundisho yangu na hivyo kwa sasa wakati huu bila shaka nitakuwa na mawasiliano ya wazi zaidi na dada huyu na kufikia uhusiano wa kufanya kazi wenye kuridhisha.