7/06/2018

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II - Maonyesho Mahususi ya Kumcha Mungu kwa Ayubu na Kujiepusha na Maovu katika Maisha Yake ya Kila siku

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II - Maonyesho Mahususi ya Kumcha Mungu kwa Ayubu na Kujiepusha na Maovu katika Maisha Yake ya Kila siku

Kanisa la Mwenyezi Mungu,  Umeme wa Mashariki, Kazi ya Mungu

Maonyesho Mahususi ya Kumcha Mungu kwa Ayubu na Kujiepusha na Maovu katika Maisha Yake ya Kila siku

Kisha, hebu tuangalie maonyesho mahususi ya kumcha Mungu kujiepusha na maovu kwa Ayubu. Juu ya vifungu hivi vinavyotangulia na kufuata, hebu pia tusome Ayubu 1:5, ambayo ni mojawapo ya maonyesho mahususi ya kumcha Mungu na kujiepusha kwa maovu kwa Ayubu. Inahusu namna ambavyo alimcha Mungu na kujiepusha na maovu katika maisha yake ya kila siku; muhimu zaidi, hakufanya tu kile alichostahili kufanya kwa minajili ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu kwake, lakini pia mara kwa mara alitoa sadaka iliyoteketezwa mbele ya Mungu kwa niaba ya wana wake. Alikuwa na hofu kwamba walikuwa mara nyingi “wametenda dhambi, na kumlaani Mungu katika mioyo yao” wakati wakiwa na karamu. Na uoga huu ulijionyesha vipi ndani ya Ayubu? Maandishi asilia yanatupa simulizi ifuatayo: “Na ilikuwa hivyo, hizo siku za karamu zao zilipokuwa zimetimia, Ayubu aliwatuma na kuwatakasa, kisha akaamka asubuhi na mapema, na kutoa sadaka za kuteketezwa kulingana na hesabu yao wote ilivyokuwa.” Mwenendo wa Ayubu unatuonyesha kwamba, badala ya kuonyeshwa katika tabia yake ya nje, kumcha Mungu kwake kulitokea ndani ya moyo wake, na kwamba kumcha Mungu kwake kungepatikana katika kila kipengele cha maisha yake ya kila siku, wakati wote, kwani hakujiepusha na maovu tu yeye mwenyewe, lakini pia alitoa sadaka zilizoteketezwa kwa niaba ya watoto wake wa kiume. Kwa maneno mengine, Ayubu hakuwa tu mwenye hofu ya kutenda dhambi dhidi ya Mungu na kumkataa Mungu katika moyo wake, lakini pia alikuwa na wasiwasi kwamba watoto wake wa kiume walitenda dhambi dhidi ya Mungu na kumkataa Yeye katika mioyo yao. Kutokana na haya ukweli unaweza kuonekana kwamba ukweli wa kumcha Mungu kwa Ayubu unapita uchunguzi, na ni zaidi ya shaka ya binadamu yeyote. Je, alifanya hivi mara kwa mara, au mara nyingi? Sentensi ya mwisho ya maandishi ni “Hivyo ndivyo Ayubu alivyofanya siku zote.” Maana ya maneno haya ni kwamba Ayubu hakuenda na kuangalia watoto wake mara kwa mara au wakati alipenda kufanya hivyo, wala hakutubu kwa Mungu kupitia kwa maombi. Badala yake, aliwatuma mara kwa mara na kuwatakasa watoto wake wa kiume kutoa sadaka iliyoteketezwa kwa niaba yao. Hiyo kauli “bila kusita” hapa haimaanishi alifanya hivyo kwa siku moja au mbili, au kwa muda mfupi tu. Inasema kwamba maonyesho ya kumcha Mungu kwa Ayubu hayakuwa ya muda, na hayakusita kwa maarifa aliyokuwa nayo au kwa maneno aliyotamka; badala yake, njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu iliongoza moyo wake, iliamuru tabia yake, na ilikuwa, ndani ya moyo wake mzizi wa uwepo wake. Kwamba alifanya hivyo bila kusita yaonyesha kwamba, katika moyo wake, mara nyingi alikuwa na hofu kwamba yeye mwenyewe angetenda dhambi dhidi ya Mungu na alikuwa na wasiwasi pia kwamba watoto wake wa kiume na binti zake walitenda dhambi dhidi ya Mungu. Inawakilisha namna tu ambavyo uzito wa njia ambayo alimcha Mungu na kujiepusha na maovu ulibebwa ndani ya moyo wake. Alifanya hivyo bila kusita kwa sababu, ndani ya moyo wake, alikuwa na hofu na wasiwasi—wasiwasi kwamba alikuwa ametenda maovu na kutenda dhambi dhidi ya Mungu, na kwamba alikuwa amepotoka kutoka kwenye njia ya Mungu, na basi alikuwa hawezi kutosheleza Mungu. Wakati huohuo, alikuwa pia na wasiwasi kuhusu watoto wake wa kiume na binti zake, akiogopa kwamba walikuwa wamemkosea Mungu. Hivyo ndivyo ulivyokuwa mwenendo wa kawaida wa Ayubu katika maisha yake ya kila siku. Kwa hakika ni mwenendo wa kawaida ambao unathibitisha kwamba kumcha Mungu na kujiepusha kwa maovu kwa Ayubu si maneno matupu tu, kwamba Ayubu aliishi kwa kudhihirisha kwa kweli ukweli kama huo. “Hivyo ndivyo Ayubu alivyofanya siku zote”: Maneno haya yanatuambia kuhusu matendo ya kila siku ya Ayubu mbele ya Mungu. Alipofanya hivi bila kusita, tabia yake na moyo wake vilifika mbele ya Mungu? Kwa maneno mengine, Mungu mara nyingi alipendezwa na moyo wake na tabia yake? Basi, ni katika hali gani na katika muktadha gani Ayubu alifanya hivi bila kusita? Baadhi ya watu wanasema kwamba ilikuwa ni kwa sababu Mungu alijitokeza kwa Ayubu mara kwa mara na ndiyo maana akatenda hivi; baadhi wanasema kwamba alifanya hivi bila kusita kwa sababu angejiepusha na maovu; na baadhi wanasema kwamba alifikiria kwamba utajiri wake ulikuwa haujaja kwa urahisi, na alijua kwamba alikuwa amepewa na Mungu, na hivyo alikuwa na uoga mwingi wa kupoteza mali yake kutokana na kutenda dhambi dhidi ya au kumkosea Mungu. Je, yapo madai yoyote kati ya haya yaliyo kweli? Bila shaka la. Kwani, kwa macho ya Mungu, kile Mungu amekubali na kupenda sana kuhusu Ayubu si tu kwamba alifanya hivi bila kusita; zaidi ya hapo, ilikuwa ni mwenendo wake mbele ya Mungu, binadamu, na Shetani alipokabidhiwa Shetani na kujaribiwa. Sehemu zilizo hapa chini zinatupa ithibati yenye ushawishi mkubwa zaidi, ithibati ambayo inatuonyesha ukweli wa ukadiriaji wa Mungu kwa Ayubu. Kinachofuata, hebu tusome maandiko kwenye vifungu vifuatavyo.

2. Shetani Anamjaribu Ayubu kwa Mara ya Kwanza (Mifugo Yake Yaibiwa na Janga Lawapata Watoto Wake)
a. Maneno Yaliyotamkwa na Mungu
(Ayubu 1:8) Je, umemwangalia mtumishi wangu Ayubu, kwa kuwa hakuna hata mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuuepuka uovu?
(Ayubu 1:12) BWANA akamwambia Shetani, Tazama, yote aliyo nayo yamo katika uwezo wako; lakini usinyoshe mkono wako juu yake yeye mwenyewe. Basi Shetani akatoka mbele za uso wa BWANA.
b. Jibu la Shetani
(Ayubu 1:9-11) Kisha Shetani akamjibu BWANA, akasema, Je, Huyo Ayubu anamcha BWANA bure? Wewe hujamzingira kwa ukigo pande zote, na kwa nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo kwa kila upande? Umezibariki kazi za mikono yake, na mali yake imeongezeka katika nchi. Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, na yeye atakukufuru mbele ya uso wako. 
...
Juni 13, 2014

Tanbihi:

a. Maandishi asilia yanasoma “vitendo.”

b. Maandishi asilia yameacha “kichwa cha.”

c. Maandishi asilia yameacha “kupotezwa kwa.”

d. Maandishi asilia yameacha “ yaliyokuwa yameenda.”

e. Mtu/kitu kinachodhihirisha uzuri/ubora wa kingine kwa kuvilinganisha.

kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni