5/28/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 60

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 60

Si jambo rahisi kwa maisha kukua; yanahitaji mchakato, na aidha, kwamba muweze kulipa gharama na kwamba mshirikiane na Mimi kwa uwiano, na hivyo mtapata sifa Yangu. Mbingu na dunia na vitu vyote vinaanzishwa na kufanywa kamili kupitia maneno ya kinywa Changu na chochote kinaweza kutimizwa nami. Matakwa Yangu ya pekee ni kwamba mkue haraka, mchukue mzigo kutoka kwa mabega Yangu na kuuweka kama wenu, mfanye kazi Zangu kwa niaba Yangu, na hilo litauridhisha moyo Wangu.

5/27/2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja” Sehemu ya Pili



Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja”  Sehemu ya Pili

  
Mwenyezi Mungu anasema, “Mungu aliumba binadamu na Akawaweka duniani, ambao Amewaongoza mpaka siku ya leo. Kisha Akaokoa binadamu na kuhudumu kama sadaka ya dhambi kwa binadamu. Mwishowe lazima bado ashinde binadamu, aokoe binadamu kabisa na kuwarejesha kwa mfano wao wa awali. Hii ndiyo kazi Amekuwa akifanya kutoka mwanzo hadi mwisho—kurejesha mwanadamu kwa sura yake halisi na kwa mfano wake wa awali.

5/26/2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 59

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Maneno ya Mungu | Sura ya 59

Tafuta mapenzi Yangu zaidi katika mazingira unayoyakabili na kwa hakika utapata kibali Changu. Ilmradi uwe tayari kwenda katika utafutaji na kuhifadhi moyo ambao unanicha, Mimi Nitakupea yote unayokosa. Kanisa sasa linaingia utendaji rasmi na mambo yote yanaingia kwenye alama sahihi. Mambo hayako yalivyokuwa wakati mlipokuwa na limbuko la mambo yajayo. Lazima msiwe wa kuchanganyikiwa au kuwa bila utambuzi.

5/25/2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 58

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Sauti ya Mungu | Sura ya 58

Ukiielewa nia Yangu, utaweza kuufikiria mzigo Wangu na unaweza kupata mwanga na ufunuo, na kupata ufunguliwaji na uhuru, kuuridhisha moyo Wangu, kuyaruhusu mapenzi Yangu kwa ajili yako kutekelezwa, kuwaletea watakatifu wote ujenzi wa maadili, na kuufanya ufalme Wangu duniani kuwa imara na thabiti. Jambo la muhimu sasa ni kuelewa nia Yangu, hii ni njia mnayopaswa kuingia katika na hata zaidi ni wajibu wa kutimizwa na kila mtu.

5/24/2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 57

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Maneno ya Mungu | Sura ya 57

Je, umechunguza kila fikira na mawazo yako, na kila tendo lako? Uko wazi kuhusu gani kati ya haya yanalingana na mapenzi Yangu na gani hayalingani? Huna uwezo wa kutambua haya! Mbona hujaja mbele Yangu? Je, ni kwa sababu Sitakuambia, au ni kwa ajili ya sababu nyingine? Unapaswa kujua hili! Kujua kwamba wale walio wazembe hawawezi kuyaelewa mapenzi Yangu kabisa au kupokea mwangaza na ufunuo mkuu.

5/23/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 56

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 56

Nimeanza kuchukua hatua kuadhibu wale ambao hufanya uovu, wale ambao hushika madaraka, na wale ambao hutesa wana wa Mungu. Kuanzia sasa kuendelea, yeyote anayenipinga katika moyo wake, mkono wa amri Zangu za utawala utakuwa daima juu yake. Fahamu hili! Huu ndio mwanzo wa hukumu Yangu na hakutakuwa na huruma itakayoonyeshwa kwa yeyote na hakuna atakayesamehewa kwani Mimi ni Mungu asiye na hisia ambaye hutenda haki; ingekuwa vyema kwenu kutambua hili.

5/22/2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 55

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Maneno ya Mungu | Sura ya 55

Mwenyezi Mungu anasema: Ubinadamu wa kawaida ambao huzungumziwa si wa mwujiza sana kama watu wanavyofikiria, lakini unaweza kuvuka mipaka ya mafungo ya watu wote, matukio, na vitu, kupita mipaka ya nguvu za mazingira, na unaweza kunikaribia Mimi na kuwasiliana kwa karibu na Mimi mahali popote na katika mazingira yoyote. Ninyi daima hutafsiri vibaya nia Zangu. Ninaposema mnapaswa kuishi kwa kudhihirisha ubinadamu wa kawaida, mnajizuia na kudhibiti miili yenu.