Maneno ya Mungu | Sura ya 64
Unapaswa kutoelewa neno Langu kwa njia ya upuuzi; unapaswa kuelewa maneno Yangu kwa kuangalia vipengele vyote na unapaswa kujaribu kuyaelewa zaidi na kuyafikiri sana kwa kurudia, sio tu kwa siku ama usiku mmoja. Hujui mahali ambapo mapenzi Yangu yapo ama ni katika kipengele kipi Nalipia gharama Yangu ya bidii za kazi; unawezaje kuyazingatia mapenzi Yangu? Ninyi watu wote mko hivi; hamna uwezo wa kuchunguza kwa utondoti, mkisisitiza tu sehemu ya juu na mkiwa tu na uwezo wa uigaji.