7/07/2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 91

Sauti ya Mungu | Sura ya 91

Roho Wangu huongea na kutamka sauti Yangu daima—wangapi kati yenu wanaweza kunijua Mimi? Kwa nini lazima Nipate mwili na kuja kati yenu? Hili ni fumbo kubwa. Ninyi mnanifikiria kuhusu Mimi na kunitamani sana siku nzima, na mnanisifu, kunifurahia na kunila na kuninywa kila siku, na ilhali leo bado hamnijui Mimi. Ninyi ni wajinga na vipofu kweli! Jinsi gani mnavyonijua kidogo! Ni wangapi kati yenu wanaweza kufikiria kuhusu mapenzi Yangu?

7/06/2019

Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | “Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja” sehemu ya kwanza



Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu  | “Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja” sehemu ya kwanza

Mwenyezi Mungu anasema, “Kuingia rahani hakumaanishi kwamba mambo yote yatakoma kusonga, ama kwamba mambo yote yatakoma kuendelea, wala hakumaanishi kwamba Mungu atakoma kufanya kazi ama mwanadamu atakoma kuishi. Ishara ya kuingia rahani ni kama hii: Shetani ameangamizwa; wale watu waovu wanaomuunga mkono Shetani kwa kufanya maovu wameadhibiwa na kuondolewa; nguvu zote za uhasama kwa Mungu zimekoma kuwepo.

7/05/2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)” Sehemu ya Tatu



Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X  Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)” Sehemu ya Tatu


3. Mzunguko wa Uhai na Mauti wa Watu Wanaomfuata Mungu


Mwenyezi Mungu anasema,"Baada ya hayo, hebu tuzungumzie mzunguko wa uhai na mauti wa wale wanaomfuata Mungu. Hili linawahusu, hivyo kuweni makini. Kwanza, fikiria kuhusu ni makundi gani ambamo watu wanaomfuata Mungu wanaweza kugawika. (Wateule wa Mungu na watendaji huduma.) Kuna mawili: wateule wa Mungu na watendaji huduma. Kwanza tutazungumza kuhusu wateule wa Mungu, ambao ni wachache.

7/04/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 90

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 90

Wote walio vipofu lazima waondoke kutoka Kwangu na wasiwepo kwa muda zaidi hata kidogo, kwani wale ambao Nataka ni wale ambao wanaweza kunijua, wanaoweza kuniona na wanaoweza kupata vitu vyote kutoka Kwangu. Na wanaoweza kweli kupata vitu vyote kutoka Kwangu ni nani? Hakika kuna wachache sana wa mtu wa aina hii na hakika watapata baraka Zangu. Nawapenda watu hawa na Nitawachukua mmoja baada ya mwingine kuwa wasaidizi Wangu wakuu, kuwa maonyesho Yangu, na Nitayafanya mataifa yote na watu wote wanisifu bila kukoma, wakishangilia bila kukoma kwa ajili yao wenyewe. 

7/03/2019

Matamshi ya Mungu | Sura ya 89

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Mungu | Sura ya 89
Sio rahisi kuwa sawa na makusudi Yangu kwa kila kitu unachofanya; sio jambo la kujilazimisha kudanganya, lakini inategemea ikiwa Nilikujalia na akili Yangu kabla ya kuumbwa kwa dunia, ambalo lilikuwa jukumu Langu. Hiki sio kitu watu wanachoweza kufanya. Nitampenda ninayempenda, na yeyote Ninayesema ni mzaliwa wa kwanza hakika ni mzaliwa wa kwanza, hii ni sawa kabisa. Unaweza kutaka kudanganya, lakini huku kutakuwa bure tu! Unadhani Sikutambui? Je, kuwa na tabia nzuri mbele Yangu inatosha?

7/02/2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 88

Sauti ya Mungu | Sura ya 88

Watu hawawezi tu kuwaza kiasi ambacho mwendo Wangu umezidisha kasi: Ni ajabu ambayo imetokea isiyoeleweka kwa mwanadamu. Tangu uumbaji wa dunia, mwendo Wangu umeendelea na kazi Yangu haijawahi kusimama. Ulimwengu wote hubadilika siku kwa siku na watu pia wanabadilika mara kwa mara. Hizi zote ni kazi Zangu, mipango Yangu yote na hata zaidi, usimamizi Wangu—hakuna mtu anayejua au kuelewa hivi vitu.

7/01/2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 87

Maneno ya Mungu | Sura ya 87

Lazima uharakishe hatua na ufanye kile Nataka kufanya. Hii ni kusudi Langu lenye hamu kwenu. Inawezekana kuwa kwa wakati huu bado hamjaelewa maana ya maneno Yangu? Inawezekana kuwa bado hamjui kusudi Langu? Nimezungumza wazi zaidi na zaidi, na kusema mengi zaidi, lakini, je, ninyi hamjajitahidi kujaribu kuelewa maana ya maneno Yangu? Shetani, usifikiri kwamba unaweza kuharibu mpango Wangu!