5/07/2018

Christian movie “Siri ya Utauwa: Mfuatano” | Preaching the Gospel of the Second Coming of Lord Jesus



Christian movie “Siri ya Utauwa: Mfuatano” | Preaching the Gospel of the Second Coming of Lord Jesus


Utambulisho

Lin Bo'en ni mhubiri mzee ambaye amemwani Bwana kwa miongo mingi. Tangu alipomkubali Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho, alihukumiwa, akatengwa, na akafukuzwa kutoka kwa jumuiya ya kidini na wachungaji na wazee wa kanisa, nguvu zinazompinga Kristo. Lakini ingawa Lin Bo’en alishambuliwa, akahukumiwa na kusingiziwa, hakusita kwa woga. Badala yake, imani yake ikawa thabiti zaidi kuliko ilivyowahi kuwa, na hili lilimwongoza kufahamu hatimaye kwamba wachungaji na wazee wa kanisa wa ulimwengu wa dini walikuwa wakiigiza kwa udanganyifu sura adilifu.

5/06/2018

Unapaswa Kupokeaje Kurudi kwa Kristo wa Siku za Mwisho?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Nyimbo ya Msifuni Mwenyezi Mungu
Nyimbo ya Msifuni Mwenyezi Mungu


Unapaswa Kupokeaje Kurudi kwa Kristo wa Siku za Mwisho?



Utambulisho

Wimbo wa Maneno ya Mungu
I
Mwili wa Mungu utajumlisha kiini cha Mungu na maonyesho Yake. Atakapofanywa mwili, Ataleta matunda ya kazi Aliyopewa ajidhihirishe na Alete Ukweli kwa wote, awape uhai na awaonyeshe njia. Mwili wowote usiokuwa na dutu Yake sio Mwili wa Mungu.

5/05/2018

"Imani katika Mungu" (1) - Je, Utiifu kwa Wale Walio Madarakani Kweli ni Sawa na Utiifu kwa Mungu?



"Imani katika Mungu" (1) - Je, Utiifu kwa Wale Walio Madarakani Kweli ni Sawa na Utiifu kwa Mungu?



Utambulisho

Katika Biblia, Paulo alisema, "Acha kila nafsi itii mamlaka ya juu zaidi. Kwani hakuna mamlaka isipokuwa ya Mungu: mamlaka yaliyoko yameamriwa na Mungu. Yeyote yule anayepinga nguvu, anapinga amri ya Mungu: na yule anayepinga atapokea laana” (Warumi 13:1-2). Sisi waumini tunapaswa kuwatendea vipi wale walio madarakani? Je, utiifu kwa wale walio madarakani ni sawa na utiifu kwa Mungu kweli?

5/04/2018

Mungu Ndiye Chanzo cha Uhai wa Mwanadamu

Mungu Ndiye Chanzo cha Uhai wa Mwanadamu

Tangu unapoingia katika dunia hii ukilia, unaanza kutekeleza wajibu wako. Unachukua jukumu lako katika mpango wa Mungu na katika utaratibu wa Mungu. Unaanza safari ya maisha. Licha ya asili yako na licha ya safari iliyoko mbele yako, hakuna kitakachoepuka mpango na utaratibu ambao mbingu imeweka, na hakuna aliye na udhibiti wa hatima yake, kwa maana Anayetawala juu ya kila kitu ndiye tu Aliye na uwezo wa kazi hiyo. Tangu siku aliyoumbwa binadamu, Mungu amekuwa thabiti katika kazi Yake, kusimamia ulimwengu huu na kuelekeza mabadiliko na harakati ya mambo yote.

5/03/2018

Christian Video Swahili “Bahati na Bahati Mbaya” | Mshukuru Mungu kwa Neema Yake ya Ajabu



Christian Video Swahili “Bahati na Bahati Mbaya” | Mshukuru Mungu kwa Neema Yake ya Ajabu


Utambulisho

Kwa sababu yeye alitoka katika familia iliyo masikini, tangu akiwa na umri mdogo Du Juan alikusudia kutengeneza pesa nyingi sana apate kuishi maisha mazuri. Ili kufikia lengo hili, aliacha shule mapema zaidi kwenda kufanya kazi ya mikono, chochote angeweza kufanya ili apate pesa. Yeye hakulalamika wakati kazi ilikuwa ngumu na ya kuchokesha.

5/02/2018

Swahili Gospel Praise Music "Kila Kitu Kinaishi Chini ya Sheria na Masharti Yaliyowekwa na Mungu"

 


Swahili Gospel Praise Music "Kila Kitu Kinaishi Chini ya Sheria na Masharti Yaliyowekwa na Mungu"


Utambulisho


Miaka elfu kadhaa imepita,
na mwanadamu angali anafurahia nuru na hewa aliyopewa na Mungu,
angali anapumua pumzi iliyotolewa na Mungu Mwenyewe,
angali anafurahia maua, ndege, samaki na wadudu walioumbwa na Mungu,
na kufurahia viumbe vyote vilivyotolewa na Mungu;

5/01/2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | 58. Wivu, Ugonjwa Sugu Wa Kiroho

Kanisa la Mwenyezi Mungu | 58. Wivu, Ugonjwa Sugu Wa Kiroho

He Jiejing    Jiji la Hezhou, Mkoa wa Guangxi
Dada mmoja na mimi tuliunganishwa ili tusahihishe makala pamoja. Tulipokuwa tukikutana, nilitambua kuwa haikujalisha kama ilikuwa ni kuimba, kucheza ngoma, kupokea neno la Mungu, au kuwasiliana ukweli, huyu dada alikuwa bora kuniliko katika kila kipengele. Ndugu wa kiume na wa kike wa familia mwenyeji wote walimpenda na wangezungumza naye. Kwa sababu ya hili, moyo wangu ulikuwa na wasiwasi sana na nilihisi kama nilikosa kuthaminiwa—hata kufikia kiasi kwamba nilifikiri kuwa mradi alikuwa huko, hakukuwa na nafasi yangu.